NAMNA YA KUFAHAMU KITAMBULISHO CHAKO CHA NIDA KAMA KIMEKAMILIKA NA MAHALI PA KUKIPATA KUPITIA SIMU YAKO
Habari mpendwa msomaji wa Makala hii, kama umekua ukijiuliza ni namna gani unaweza kujua kama kitambulisho chako cha Taifa (NIDA) kiko tayari au la na je! Ni mahali gani unaweza kwenda kukichukua ili uanze kukitumia kwa matumizi ya kila siku basi uko mahala sahihi kwasababu nitakuelekeza hatua kwa hatua hadi utafanikiwa kukipata kwa kutumia computer au simu yako ya mkononi.
MAANA YA KITAMBULISHO CHA TAIFA
Kitambulisho cha Taifa ni nakala inayoelezea taarifa muhimu za raia wa Tanzania kama vile jina, mahali anapoishi, jinsia na umri wake. Vitambulisho hivi nchini Tanzania hutolewa na mamlaka husika ya vitambulisho vya Taifa au NIDA kwa ajili ya kumtambua kila raia wa hapa nchini kuwa ni mkazi wa kudumu, mkazi muhamiaji au mkimbizi.
NAMNA YA KUFAHAMU KITAMBULISHO CHAKO KAMA KIKO TAYARI NA WAPI UTAWEZA KUKIPATA
Katika Makala iliyopita tulieleza namna unaweza kufahamu namba yako ya kitambulishocha Taifa na sasa tunaenda kuangalia ni mahali gani unaweza kukipata kitambulisho chako bila gharama yoyote. Kabla ya kuanza unapaswa kuwa na vitu vifuatavyo ;
1. Jina ulilotumia kujisajili yaani jina la mwanzo, jina la kati na jina la mwisho.
2. Mahali ambapo ulienda kuandikisha taarifa zako za kitambulisho yaani Mkoa, Wilaya, Kata na Mtaa.
Baada ya kuwa unafahamu hivo vitu viwili sasa utachukua simu yako au computer na kuingia kwenye kivinjari chochote nashauri Zaidi utumie Google Chrome kwasababu ni rahisi na inauwezo wa kufungua kurasa nyinyi bila usumbufu. Baada ya kufungua kivinjari chako sasa ingia tovuti ya mamlaka ya vitambulisho vya Taifa kwa kusearch au kuandika kubonya kiungo hiki https://nida.go.tz/ hapa moja kwa moja utatokea ukurasa wa mamlaka ya vitambulisho vya taifa kama inavyoonekana hapa chini.
Baada ya ukurasa wa NIDA kufunguka angalia upande wa juu kulia na tafuta maneno yaliyoandikwa KITAMBULISHO CHA TAIFA na kisha bonyeza na uchague FAHAMU KITAMBULISHO KILIPO.
Kisha itatokea hapa…
Baada ya hapo gusa mkoa ulipojiandikishia taarifa zako, kisha gusa wilaya na mwisho kabisa gusa kata / kijiji kama unavoelekezwa na mfumo. Baada ya kumaliza hatua hizo zote yatatokea majina ya watu mbalimbali waliojiandikisha kata hiyo na utafute jina lako kulingana na herufi yako ya mwanzo. Mf. Joshua utashuka hadi ilipoanzia herufi J.
Kumbuka; majina pekee utakayoyaona katika ukurasa wa mwisho ni ya wale ambao vitambulisho vyao vimekamilika kwa mfumo wa hardcopy tu (yaani vitambulisho vyao vimeshachapishwa) na kutumwa kwenye ofisi husika. Hii inamaanisha kama usipoliona jina lako na namba ya NIDA unayo basi fahamu ya kuwa kitambulisho chako bado hakijachapishwa kwa mfumo wa hardcopy. Pia kuwa makini katika uchaguzi wa kata maana watu wengi husahau mahali halisi walipojiandikisha hivyo unashauriwa kuangalia jina lako na kata za jirani laweza kuwa humo.
Aidha kama utapenda kuingia mwenyewe moja kwa moja kwenye tovuti ya vitambulisho vya Taifa kwa njia fupi ni rahisi sana bonyeza kiungo hiki (https://vitambulisho.nida.go.tz/) na kisha fuata hatua zote kama ilivyoelezwa hapo juu kujua kama kitambulisho chako kimetokaau lah.
TAFADHALI USISITE KUACHA COMMENT YAKO MAHALI POPOTE ULIPOKWAMA AU PATA CHANGAMOTO.
Comments
Post a Comment