Skip to main content

FAHAMU NAMBA YAKO YA NIDA (NIN) MTANDAONI KIURAHISI

UTANGULIZI

Namba ya NIDA (National Identification Number i.e. NIN) ni namba ambayo anapewa raia wa nchi ya Tanzania baada ya kujiandikisha kwenye serikali yake ikiwa kama utambuzi wa uraia wake nchini. Namba hii inapatikana katika kitambulisho cha Taifa cha uraia kwa raia wote wa Tanzania na hutumika katika shughuli mbalimbali za kijami na kiserikali ndani na nje ya nchi.

Ni muhimu kwa kila raia kuwa na kitambulisho cha Taifa (NIDA), lakini kutokana na ugumu wa utengenezaji wa vitambulisho hivi kumekua na uchelewaji wa utengenezaji wa nakala halisi ya kitambulisho na kupelekea raia wengi kutumia tu namba zilizopo kwenye kitambulisho hicho kwa kujisajili katika huduma mbalimbali pindi wanaposubiri nakala halisi ya vyeti vyao.

Baadhi ya watu wamekuwa wakijiuliza ni namna gani wanaweza kuipata namba hii bila ya kwenda ofisi ya serikali au mtaa walipojiandikisha!. Bahati nzuri kutokana na mabadiliko ya kukua kwa sayansi na teknolojia serikali kupitia wizara yake imetengeneza website ambayo itamuwezesha raia yeyote kujipatia huduma anayotaka kuhusu kitambulisho chake cha Taifa (NIDA) bila gharama yeyote ile iwapo atakua na kifaa chochote kitakachomuwezesha kufanya ivo yani simu janja (smartphone) au computer. Baadhi ya huduma hizo ni upataji wa namba ya NIDA na kivuli cha nakala ya kitambulisho chake ambayo kwasasa imesitishwa.

 

MAMBO MUHIMU YA KUYAFAHAMU KABLA HUJAOMBA NAMBA YAKO YA NIDA;-

1.      Kutambua majina ya muombaji yaani jinala kwanza na jina la ukoo.

2.      Kutambua tarehe, mwezi na mwaka aliozaliwa muombaji.

3.      Kutambua majina ya mama wamuombaji yaani jina la kwanza na la mwisho la mama wa muombaji.

4.      Kuweza kutambua na kuandika msimo wa namba za usalama zitakazotolewa na mfumo ili kuthibitisha kuwa muombaji sio robot.

NB: KUMBUKA KUJAZA NAMBA ZA USALAMA UTAKAZOPEWA NA MFUMO CHINI YA FOMU YA UJAZAJI KAMA ZILIVO KWA KUANGALIA NAMBA, ALAMA, HERUFI KUBWA NA NDOGO NA ENDAPO UTAKOSEA BASI REFRESH BROWSER YAKO ILI UWEZE KUPEWA NAMBA ZINGINE.

 


 HATUA ZA KUFUATA ILI UWEZE KUTAMBUA NAMBA YA NIDA

Ili uweze kufahamu kikamilifu namba yako ya NIDA kwanza kabisa hakikisha una kifurushi cha MB na ni lazima ufuate kiumakini hatua zifuatazo bila kuacha hata kipengele kimoja. Hatua izo ni ;-

1.     1.Ingia kwenye browser ya computer yako au simu janja , unashauriwa kutumia browser yenye uzoefu mkubwa ya Google Chrome.



 

2.Katika sehemu ya search andika (services.nida.go.tz/nidportal/get_nin.aspx) au bonyeza kiungo hiki >>> FAHAMU NAMBA YANIDA


3.
Baada ya fomu ya kuomba namba ya NIDA kujitokeza utatakiwa kujaza kama fomu inavyoeleza yaani majina na tarehe ya kuzaliwa na bila kusahau kumalizia na neno lililojizalisha chini ya fomu na mwishoni bonyeza neno Tuma ili kuipata namba yako.



Baada ya kumaliza kujaza kila kitu utaona namba yako ya NIDA ikijitokeza kwenye box mstari wa chini kabisa ya page yako ikianzia na mwaka wa kuzaliwa, mwezi wa kuzaliwa na tarehe, namba ya fomu na namba zingine kukamilisha namba zote zakitambulisho cha uraia.



Bila shaka utakua umefuata na kufanikiwa kirahisi kabisa kutambua namba yako ya NIDA kwa njia ya mtandao. Tafadhali endelea kufuatilia makala yetu kujua mengi yanayojiri na kujifunza mambo mbalimbali yanayoendelea nchini na duniani kuhusu elimu na teknolojia pia kumbuka kutuachia maoni yako hapa chini, ahsante.

Comments

Popular Posts

JINSI YA KUTAZAMA MATOKEO YA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2026 MTANDAONI; MUONGOZO KAMILI KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI

  Matokeo ya Kidato cha Pili ni hatua muhimu sana katika maisha ya mwanafunzi wa sekondari Tanzania. Matokeo haya yanatoa taarifa kuhusu ufanisi wa mwanafunzi baada ya kumaliza mwaka wa pili wa masomo, na ni muhimu kwa hatua zinazofuata kama kujiandaa kwa kidato cha tatu au mikakati ya kuboresha ufaulu katika masomo mbalimbali. Matokeo haya yanatolewa rasmi na National Examinations Council of Tanzania ( NECTA ) kupitia njia mbalimbali, ikiwemo mtandao.  NECTA ni Nini? Na Kwa Nini Matokeo ya Kidato Cha Pili ni Muhimu? NECTA ni chombo kinachosimamia mitihani ya kitaifa Tanzania, ikijumuisha mitihani ya darasa la saba, kidato cha pili, kidato cha nne, kidato cha sita na mingineyo. Matokeo ya Kidato cha Pili (inayojulikana kama Form Two National Assessment – FTNA ) hutolewa kila mwaka baada ya mtihani kufanyika mwishoni mwa mwaka wa masomo. Matokeo haya ni muhimu kwa sababu: Huonyesha mahali mwanafunzi amesimama kitaaluma baada ya miaka miwili ya sekondari, husaidia watahiniwa, ...

HIGHLIGHTS 4 - 1: ARSENAL YAIPA KIPIGO KIKALI ASTON VILLA NA KUBAKIA KILELENI EPL

🔴⚪ ARSENAL WATHIBITISHA UBABE DHIDI YA ASTON VILLA BAADA YA USHINDI MNONO WA 4–1 Tarehe : 30 Desemba 2025 Uwanja : Emirates Stadium Arsenal waliendelea kuonyesha dhamira yao ya kupigania mafanikio makubwa msimu huu baada ya kuichapa Aston Villa kwa mabao 4–1 katika mechi ya kusisimua iliyochezwa kwenye Uwanja wa Emirates . Ilikuwa ni mechi iliyojawa na kasi, ushindani mkubwa na burudani ya hali ya juu, huku Arsenal wakithibitisha kwa vitendo kuwa wako katika kiwango cha juu sana. 🕒 MWANZO WA MECHI : ARSENAL WANZA KWA KASI Mara tu baada ya kipenga cha kuanza kusikika, Arsenal waliingia kwa kasi kubwa wakitawala umiliki wa mpira na kuwabana Aston Villa katika eneo lao. Mfumo wa pasi fupi, presha ya juu ( high press ) na kusogea kwa pamoja kuliwapa Arsenal udhibiti wa mchezo mapema. Leandro Trossard , aliyekuwa akicheza upande wa kushoto, alianza kuwasumbua mabeki wa Villa kwa mbio za kasi, dribbling za kuvutia na kupandisha mashambulizi mara kwa mara. ⚽ GOLI LA KWANZA : ...

LIVERPOOL WAANZA MWAKA KWA SARE TASA: LEEDS UNITED WAWEKA KAMBI ANFIELD

UTANGULIZI Mwaka mpya wa 2026 umeanza kwa mtindo wa kipekee katika Ligi Kuu ya England, ambapo Liverpool na Leeds United walikutana Anfield na kuishia kwa sare tasa ya 0-0. Mashabiki wa Reds walitarajia kuona mwanzo wa kishindo chini ya kocha Arne Slot , lakini ukuta wa Leeds uliosimamiwa na Daniel Farke ulihakikisha hakuna mabao yaliyopatikana. Hii ilikuwa mechi ya kwanza ya mwaka na pia clean sheet ya kwanza kwa Leeds tangu Agosti, ikitoa taswira ya nidhamu na uimara wa kiulinzi dhidi ya moja ya timu kubwa zaidi nchini. Muhtasari wa Mechi - Tarehe na Mahali : 1 Januari 2026, Anfield   - Matokeo : Liverpool 0-0 Leeds United   - Kocha Liverpool : Arne Slot   - Kocha Leeds : Daniel Farke   Mambo Muhimu ya Mechi - Udhibiti wa mchezo: Liverpool walimiliki mpira kwa 69% lakini walishindwa kutengeneza nafasi safi za kufunga.   - XG (Expected Goals): Liverpool walitengeneza takribani 1.96xG, ikionyesha walikuwa na nafasi lakin...